iqna

IQNA

IQNA – Naibu Waziri wa Utamaduni na Mwongozo wa Kiislamu Iran ambaye anasimamia masuala ya Qur'ani na Itrah amelaani vitendo vya hivi karibuni vya uchokozi vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran na kusisitiza azma ya jumuiya ya Qur'ani nchini kufungamana na utamaduni wa muqawama (mapambano ya Kiislamu) na kuupinga utawala wa Kizayuni sambamba na kutetea maadili ya Kiislamu.
Habari ID: 3480838    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/15

IQNA — Zaidi ya nakala milioni mbili za Qur'ani Tukufu zinasambazwa miongoni mwa Mahujaji wanaorejea nyumbani baada ya ibada ya Hija nchini Saudi Arabia.
Habari ID: 3480816    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/10

Hija Katika Qur’ani/9
IQNA – Qur’ani Tukufu inawakumbusha Watu wa Kitabu (Ahlul Kitab), wanaojinasibu kuwa wafuasi wa Nabii Ibrahim (AS), kuwa ikiwa madai yao ni ya kweli, basi wanapaswa kuamini msingi wa Ibrahimu katika ujenzi wa Kaaba na kuitambua kama Qibla (eneo la kuelekea wakati wa swala) ya kweli ya Mwenyezi Mungu.
Habari ID: 3480814    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/09

IQNA – Makumbusho mapya yanayolenga kuhifadhi kumbukumbu adimu za Qiraa au usomaji wa Qur'ani wa maqari maarufu wa Misri yanatarajiwa kufunguliwa katika jengo la kihistoria la Maspero jijini Cairo, katika makao ya redio na televisheni ya taifa.
Habari ID: 3480812    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/09

IQNA – Maonesho ya kudumu katika Makumbusho ya Qur'ani jijini Makkah yanawapa wageni tajiriba ya kipekee ya kiutamaduni na kiroho kupitia hati nadra za Qur'ani na nakala kubwa zaidi ya Qur'ani duniani.
Habari ID: 3480811    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/09

IQNA – Jumuiya ya Waislamu Duniani (MWL) imekaribisha uamuzi wa mahakama ya Uingereza kumtia hatiani mtu aliyeteketeza moto nakala ya Qur’ani Tukufu mjini London. 
Habari ID: 3480807    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/08

IQNA – Kitabu kipya kilichoandikwa kuhusu sayansi ya Qur’ani kimetangazwa rasmi kama rasilimali ya elimu kwa wanafunzi wa kiwango cha kwanza katika vyuo vya Kiislamu kote Iran.
Habari ID: 3480806    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/08

IQNA – Toleo la mwaka 2026 la Tuzo ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu ya Dubai litaandaliwa chini ya dira mpya iliyopewa kauli mbiu: "Katika Kutafuta Qiraa Nzuri Zaidi ya Qur’ani Tukufu."
Habari ID: 3480795    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/06

Mwanazuoni
IQNA – Afisa mmoja wa Kiirani amesema kuwa hakuna njia nyingine ya kuokoa ubinadamu ila kwa kufuata mwongozo wa Qur'ani Tukufu.
Habari ID: 3480794    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/06

Hija Katika Qur'ani /8
IQNA-Katika maneno matukufu ya Qur’ani, Mwenyezi Mungu anaitambulisha Kaaba kama nyumba ya kwanza iliyoanzishwa kwa ajili ya ibada ya Mola Mmoja wa kweli. Katika Surah Aal Imran, aya za 96-97, utukufu na umuhimu wa nyumba hii takatifu vinaelezwa wazi:
Habari ID: 3480792    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/05

Hija Katika Qur'ani / 6
IQNA – Qur'ani Tukufu inawasilisha ibada za Hija kama fursa adhimu ya kujiimarisha kimaadili, kufanya mazoezi ya kujizuia, na kuandaa zana za kiroho kwa ajili ya maisha ya Akhera. Hii ni fursa isiyokadirika kwa kila Muislamu anayetafuta ukaribu na Mola wake.
Habari ID: 3480780    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/03

IQNA – Mufti Mkuu wa Misri amesisitiza kwamba kuhifadhi Qur’ani Tukufu hakupaswi kuishia katika kurudia na kukariri pekee, bali kunapaswa kuwa mchakato wa makusudi unaoambatana na kutafakari maana ya aya.
Habari ID: 3480778    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/02

IQNA – Toleo la tatu la mpango wa majira ya joto wa Qur'ani wa Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar nchini Misri limeanza kutekelezwa Jumapili.
Habari ID: 3480774    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/01

IQNA – Ibada ya Hija ni fursa adhimu kwa wasomaji wa Qur'ani kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu kukutana, kushirikiana na kunufaika na tajiriba za wenzao, amesema Qari mmoja kutoka Iran.
Habari ID: 3480771    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/01

IQNA – Rais wa Nigeria ameielezea Qur'ani Tukufu kama mwongozo kamili kwa wanadamu na chanzo cha nuru, hekima na faraja.
Habari ID: 3480770    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/01

IQNA – Jukwaa la Sayansi ya Qur'ani, linaloendeshwa na Idara ya Mfawidhi wa Haram Takatifu ya Hadhrat Abbas (AS) huko Karbala, Iraq, limezindua toleo la 9 la mpango wa kitaifa wa Qur'ani.  
Habari ID: 3480766    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/31

IQNA-Mkuu wa Mamlaka ya Kitaifa ya Vyombo vya Habari ya Misri ametangaza mipango ya kuzindua Jumba la Makumbusho ya Wasomaji wa Qur'ani nchini humo.
Habari ID: 3480765    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/31

IQNA-Wanazuoni wa Kiislamu hivi karibuni wameanzisha mradi kwenye mitandao ya kijamii uitwao "Darasa za Qur’ani", wenye lengo la kukuza uelewa wa dhana za Qur’ani kwa njia inayoambatana na zama za kidijitali na teknolojia.
Habari ID: 3480763    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/30

IQNA: Qur’ani Tukufu ina maarifa ya kimataifa yanayopaswa kufafanuliwa, na ujumbe wake unapaswa kuwasilishwa kwa ulimwengu mzima, amesema Hujjatul Islam Mohsen Qara’ati, mwanazuoni wa Kiislamu na mtafsiri wa Qur’ani kutoka Iran.
Habari ID: 3480759    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/30

Hija katika Qur’ani Tukufu /5
IQNA – Qur’an Tukufu haioneshi Hija tu kama faradhi ya mtu binafsi, bali pia kama mkusanyiko mkubwa wa pamoja wenye faida kwa mtu mmoja mmoja na kwa jamii kwa ujumla.
Habari ID: 3480757    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/30